BARUA YA MUZUNGUKO Aprili 2012
Tangu mwanzo, Bwana Mungu Alijifunuwa kwa waliyo wake kwa namna mbalimbali. Kwanza katika shamba la edeni, aliwatembeleya Adamu na Eva hewa ya jioni ilikuwa ikiambatana nao (Mwanzo 3). Imeelezwa ya kama Henoc akatembea pamoja na Mungu akapokea ushuhuda ya kwamba alikubaliwa na Mungu kisha akanyakuliwa (Mwanzo 5:24; Waebrania 11:5). Tunasoma kuhusu Noa, ukamilifu wa agano nyuma ya garika na ile upinde kama alama ya agano (Mwanzo 9) na kuhusu Abrahamu ambaye kwake alipewa ahadi na kubariki mataifa yote ambayo itaamini sawa na yeye. Mungu akafanya pamoja naye agano la kutahiriwa (Mwanzo 17:13). Manabii wote wa agano la kale pamoja na watumishi wote wa Mungu bila kubaguwa, walimujuwa Bwana Mungu kwa kipekee na wakatii Maagizo yake. Kwa nyakati zote za biblia, tunasoma mashuhuda kuhusu ma ufunuo za kipekee na wakatii maagizo zake. Katika nyakati zote za Biblia, tunasoma mashuhuda zote za ufunuo za Mungu kama vile Muumbaji, Mufalme, Mukombozi, na kazalika. Katika agano jipya tunapata ufunuo ya kipekee kuhusu Mungu ndani ya Mukombozi wetu, ambaye kupitia Yeye tuliweza kufanywa wana yeye akiwa Mwana (Wagalatia 4:4-7). Anajifunuwa Yeye Mwenyewe katika vyeo vyake vyenye maana kulingana na mupango ya wokovu ya Kiungu Yeye kama Kondoo wa Mungu, Mupatanishi, Mutetezi, na kazalika.
Shabaha mukubwa ya maandishi haya ni kuonyesha ya kwamba Bwana alijifunua yeye Mwenyewe kwa wakati yetu kupitia huduma ya ndugu Branham kwa namna ile ile Aliyo jifunua katika agano la kale. Ndugu Branham aliishi ile ile mazoezi mamoja za ki maajabu ambazo walivyoishi Abraham, Musa pia manabii kwa wakati yao. Inasemaka pia kuhusu Malaika wa Bwana Alie kuwa akishuka ndani ya mwanga wakati wa maombi juu ya wagonjwa. anazungumuza mara mingi kuhusu Malaika wa agano kulingana na kutokea kwa Bwana ndani ya Nguzo ya moto ya kimaajabu. Alikuwa akisititiza akisema ya kama ilikuwa ni Ule Ule Malaika wa BWANA ambae alikuwa akisindikiza Taifa la Israeli ndani ya Wingu na katika Nguzo ya moto hapo zamani.
Mungu alijionyesha kwa Abrahamu kama vile “Malaika wa BWANA” wakati alipokuwa tayari kutowa Isaka kama zabihu, mwana wake aliye ahidiwa: “Malaika wa BWANA akamuita kutoka mbingu na kusema Abrahamuǃ Abrahamuǃ naye akajibu: mimi ni hapaǃ“ (Mwanzo 22:11-18)
Kwa wakati wa Musa, ilikuwa inahusu matokeo makubwa ya muhimu katika historia ya wokovu: wito ya kutoka na kutoka ya Taifa kama vile Mungu alivyo ahidi kwa Abrahamu (Mwanzo 15:13). “Malaika wa Bwana akamutokea katika mwanga ya moto, katika kijiti chenye kuwaka moto … Bwana akatambuwa kama alitaka kugeuka ili atazame, Mungu akamuita kutoka kijiti cha moto, na kusema: Musaǃ Musaǃ” (Kutoka 3:2+4). Hapa tuna matamshi matatu: “Malaika wa BWANA”, “BWANA” na “Mungu”, Yeye pia anajionyesha baadae kama ifutavyo: “Mimi ni Bwana Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso, kwa sababu aliogopa kuangalia Mungu” (shahiri ya 6).
Kwa umbo la Malaika, Akaonekana ndani ya mwali ya moto, kama vile Malaika, Akamuona Musa akimuzogelea, na kama Mungu Akamwambia Neno. Kwa hivyo ilihusu Yule Mmoja, kwa maana kuna Mungu Mmoja tu Ambae Alijifunuwa Yeye Mwenyewe katika agano jipya kwa ajili ya wokovu wetu, Yeye kama vile Baba mbinguni, kama vile Mwana duniani na kama Roho Mtakatifu ndani ya kanisa.
Musa alitaka amujuwe Yule ambae ana mutuma: “Musa akamwambia Mungu: ndiyo nitaenda mbele ya wana wa Israeli, na nitawaambia: Mungu wa baba zenu Ananituma kwenu. Lakini kama wakiniuliza Jina lake ni nani, nitawajibia nini? Mungu akamwambia Musa: Mimi Ndie Niko. Na akaongeza: ni hivyo utakavyo jibu wana wa Israeli: Yule Ambae Anaitwa Niko alinituma kwenu. Mungu Akamwambia tena Musa: utasema hivi kwa wana wa Israeli: Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo, Ananituma kwenu. Tazama Jina langu la milele, tazama Jina langu kizazi kwa kizazi” (Kutoka 3:13-15).
Bwana anapojifunuwa, kila mara Yeye ni NIKO. NIKO ndie Bwana, Muumbaji wa mbingu na dunia. Wakati wa kutangaza amri kumi tunasoma hivi: “Sasa Bwana Akatangaza maneno haya yote, Akisema: MIMI ni BWANA, Mungu wako… Katika Isaya 44:6, imeandikwa; “Hivi Asema Bwana, Mfalme wa Israel Ambae ni Mkombozi wake, BWANA wa majeshi: MIMI ni wa kwanza na Niko wa mwisho, na bila Mimi hakuna Mungu”. Katika wakati yote ya biblia na mpaka kitabu ya mwisho, ambacho ni cha ufunuo, BWANA Anajionesha kama MIMI NIKO. “Mimi ni alfa na omega, Asema Bwana Mungu, Yeye Ambaye Iko, Aliye kuwa, Anaye kuja, Muweza yote” (Ufunuo 1:8). “Mimi ni alfa na omega, wa kwanza na wa mwisho, mwanzo na mwisho” (Ufunuo 22:13).
Kupitia hizo “NIKO” zote ambazo Bwana Alijifunuwa ndani katika agano la kale na agano jipya, tunatambuwa ya kama kila mara ni Yeye Yule Yule. “Yesu akawaambia: kweli, kweli ninawaambia, mbele Abrahamu akuwe, Mimi Niko” (Yohane 8:58). BWANA/YAHWEH wa agano la kale Ndie BWANA YESU/YASHUAH wa agano jipya “ … na Ambaye hakuna mtu anaweza kusema: Yesu ni Bwana isipokuwa kupitia Roho Mtakatifu” (1 Wakorinto 12: 3).
Katika Yoeli 2:32 imeaandikwa: “Sasa yeye atakaye liitia Jina la BWANA/YAHWEH ataokolewa”. Katika Waroma 10:13 kunapatikana mara ingine neno lile lile kuambatana na Yesu, kwa maana atakaye liitia Jina la BWANA YESU/YASHUAH ataokolewa.
Kupitia miuziza yote ambayo Musa alifanya mbele ya Farao, kulikuwa tu shabaa moja ya kufikia: “Acha taifa langu liondoke, ili liweze kunitumikia” (Kutoka 7:26; 8:16; 9:1; 9:13; 10:3). Wakati Mungu Alipofanya agano pamoja na Israeli, hapo Bwana Akajionesha kama “Malaika wa agano”, kwa sababu kwa wakati huo alipatia taifa lake ma agizo za agano.
“Bwana Akamwaambia Musa; andika maneno haya: maana kupitia maneno haya Ninafanya agano pamoja nawe pia pamoja na Israeli. Musa akafanya pale siku makumi ine na usiku makumi ine pamoja na Bwana. Bila kula mukate, na bila kamwe kunywa maji. Na Bwana Akaandika maneno ya agano juu ya mawe, yaani ile sheria kumi” (Kutoka 34:27-28).
Kupitia Musa, Mungu akaelezea kusanyiko ambalo lilikuwa limeitwa kwa kutolewa sheria kuzifuata akasema: “Sasa, kama mukisikia sauti yangu, na ikiwa munachunga Agano langu, mutakuwa wangu kati ya mataifa zote, kwa maana dunia yote ni yangu, mutakuwa kwangu ufalme wa makuhani pia taifa takatifu. Hii ndiyo maneno utakayo waambiya wana wa Israeli” (Kutoka 19:5-6). Uwajibu ya kutowa taifa ilikuwa tu ni ya Mungu, ila pia utiifu ilibidi iongezwe kwenye Imani ya waliyo itwa, ili agano ipate kulindwa. Hivyo ndivyo kusanyiko lililo itwa kutoka likakuwa ufalme na ukahani kwa Mungu.
Na hii pia ni shabaa ya kiungu kwa wagombolewa na waliyo itwa kutoka kwenye kanisa ya agano jipya: “Lakini, ninyi, ni kabila chakuliwa, ukuhani ya ki ufalme, taifa takatifu, taifa ambalo limekubaliwa, ili mupate kutangaza mazuri ya Yule Aliye waita kutoka ndani ya giza kwa ajili ya nuru yake yenye kutukuzwa” (1. Petro 2:9). “ … uliwafanya kuwa ufalme pia makuhani wa Mungu wetu, na watatawala duniani” (Ufunuo 5:10).
Yeye kama “Malaika wa Agano”, Akaongoza taifa kwa umbo lenye kuonekana, na hii katika Wingu la kimbinguni. “Bwana alikuwa akitembea mbele yao, muchana katika nguzo ya wingu kwa kuwaongoza katika njia yao, na katika usiku katika nguzo ya moto kwa kuwaangazia, ili waweze kutembeya muchana na usiku. Nguzo ya wingu ilikuwa haichane nao mbele ya taifa kwenye muchana, ao Nguzo ya moto katika usiku” (Kutoka 13:21-22). Hivyo ndivyo Alivyo sindikiza taifa lake la Israeli muda wa myaka makumi ine.
Katika Nehemia 9:12-13, tunaambiliwa: “Ukawalinda usiku kupitia Nguzo ya wingu, na usiku kupitia Nguzo ya moto ambayo ilikuwa ikiwaangazia katika njia ambayo walikuwa wakitembeya. Ukashuka juu ya mulima wa sinai, Ukawazungumuzia juu kutoka mbingu na ukawapa maagizo ya kweli, sheria za haki, maagizo na sheria za kweli”. Bwana Mungu anaweza kujizihirisha hapa duniani akisikilizisha pia sauti yake kutoka juu mbinguni. Mungu ni Roho – Yeye ni mahali pote.
Katika Kutoka 40:33-38, Wingu inatajwa mara tano: “Hapo Wingu ikafunika hema la kusanyiko, Utukufu wa Bwana ukajaa hema la kusanyiko. Musa hangeweza kuingia ndani ya hema la kusanyiko, kwa sababu Wingu ilibaki juu, hapo Utukufu wa Bwana ukijaza hema. Wakati yote ya mwendo yao, wana wa Israeli walikuwa wanaondoka, wakati Wingu ilikuwa Ikitikisika juu ya hema. Na wakati Wingu ilikuwa haiondoke, hawangeondoka, mpaka wakati Wingu ionekane. Wingu la Bwana lilionekana muchana juu ya hema; na usiku, kama moto, kwa macho ya nyumba yote ya Israeli, katika muda ya mwendo yao.
Wakati ya uzinduo ya hekalu, Bwana Akashuka mara ingine Zaidi ndani ya Wingu la kimbinguni: “Makuhani hawakuweza kubaki kufanya kazi, kwa sababu ya Wingu; kwa sababu utukufu wa Bwana ulikuwa ukIjaa Nyumba ya Bwana” (1 Ufalme 8:10-21).