BARUA YA MUZUNGUKO Aprili 2012
Inasemeka pia kuhusu Wingu la kimbinguni katika agano jipya, kama vile wakati wa kugeuzwa sura ya Yesu kwenye mulima:
“Alipokuwa Akisema tena, Wingu lenye mwangaza likamufunika, na tazama, sauti ikatoka kwenye Wingu na kutamka maneno haya: Huyu ni Mwana wangu Mupendwa, Ambae ndani yake ninaweka mapendo yangu: mumusikilize, na Wingu likamufunika” (Matayo17:5)
Marko pia anashuhudia kuhusu tukio hilo: “Wingu likaja likawafunika, na sauti ikatoka katika Wingu: Huyu ni Mwana wangu Mupendwa: mumusikilize” (9:7).
Kulingana na kupanda yake, tunasoma katika Matendo ya Mitume 1:9-11: “Nyuma ya kusema hayo, Akanyakuliwa wakati walipokuwa wakimuangalia, wingu likamufunika kwa macho yao…”
Mukombozi wetu Alipanda mbinguni katika Wingu, na kufuatana na 1. Watesalonika 4:17, wagombolewa wote wa dunia nzima wataenda kumulaki Bwana wakiwa kwenye mawingu.
Wakati wa mazoezi ya Paulo kufuatana na wito yake, Nuru yenye kuangaa sana ikatokea mbinguni na akasikia sauti ikisema: “Sauli, Sauli, kwa nini unanitesa?” Paulo akauliza: “Wewe ni nani, Bwana? na Bwana akasema: Mimi ni Yesu unaye mutesa. Anania akatumwa kwake kulingana na maono na kusema: Saulo, ndugu yangu, Bwana Yesu, Ambaye Alikutokea njiani uliyo kuwa ukitokea, alinituma ili uweze kufungulika macho na ujazwe na Roho Mtakatifu” (Matendo ya Mitume 9:5+7b). “Mungu wa baba zetu Alikuchaguwa kujuwa mapenzi yake, kumuona mwenye haki, na kusikia maneno ya kinywa chake” (Matendo ya mitume 22:14). Katika 1 wakorinti 9:1, anashuhudia: “Mimi si huru? mimi si mutume? Je, sikumuona Yesu Bwana wetu?…” Pamoja na kuonekana ya kimbinguni ilikuwa ikifungamana na kazi ya kiungu, kutumwa ya kipekee yenye maana katika mupango ya historia wa wokovu.