BARUA YA MUZUNGUKO Aprili 2012
Katika wakati yetu pia, kumekuwa wito ambawo umehakikishwa na Mungu na kwa hiyo, ili kurudisha roho za Watoto wa Mungu kwenye Imani ya wababa wa kimitume. Hii ni utimilifu ya ahadi iliyofanywa katika Malaki 4:5-6, na ikizihirishwa na Bwana katika Matayo 17:11 na katika Marko 9:12: “Eliya atakuja kwanza, na kutayarisha vitu yote”. Ni hiyo inayo husika sasa katika kanisa la Bwana kama hapo mwanzo. Eliya akatwaa mawe 12 kulingana na kabila 12, akajenga upya mazabahu ya Bwana, akakusanya taifa juu ya mulima wa karimeli na mioyo ikarudishwa kwa Bwana (1 Wafalme 18:21-37), na hivi mtu wa Mungu wa wakati wetu alirudisha mafundisho ya wamitume 12 (Matendo ya Mitume 2:42) na kurudisha roho zetu kwa Mungu. Kanisa linapashwa rudishwa kwenye musimamo ya asili mbele Yesu aweze kurudi, kwa maana hiyo ndiyo ahadi: “Yeye Ambaye inabidi mbingu imushike mpaka nyakati za urudishaji wa vitu vyote, ambavyo Mungu alivyosema hapo zamani katika vinywa vya manabii wake watakatifu” (Matendo ya Mitume 3:21). Pia hii ni HIVI ASEMA BWANA.
Tangu utengenezaji upya, kuliwai kuwa ma uwamusho mengi ambazo shabaa kubwa ilikuwa ni mahubiri ya injili. Kwenye mwanzo ya karni ya 20 kulikuwa nguvu mpya ya Roho, ikifanana na ile ya pentekoste. Kupitia hiyo kukatokea makanisa mbalimbali ya ki pentekoste. Ijapo hivyo kulikuwa bado kuzaliwa uingiaji wa kweli katika kwenye ukristiani wa asili. Nyuma ya vita ya pili ya ulimwengu wote, kukatokea mwanaume moja mwenye huduma ya kimutume pia ya ki unabii kulingana na maandiko. Alikuwa ni William Branham, mtu aliye tumwa na Mungu kupitia yeye uwamsho mukubwa zaidi wa wokovu na wa uponyaji ukaonekana, kupita hata hapo mbele tangu siku za Yesu na za wamitume.
Tarehe 7 mwezi wa tano mwaka wa 1946, ndugu Branham akapata mazoezi ifuatayo: Kwenye saa za jioni mwanga ya kimbinguni ikitoka mbinguni ikawaka katika chumba ambacho alikuwa ndani. Ndugu Branham akaona katika mwanga huo mujumbe wa Mungu akishuka na baadae akamukaribia. Akishikwa na woga, akasimama na akasikia maneno ya kwanza: “Usiogope, nimetumwa kwako kutoka kwenye uwepo wa Mungu”. Huyu akamufasiriya kwa uhakika yote ambayo yalikuwa yakihusu huduma yake. Mara ingine akamwaambia: “Kama vile Musa alivyo pewa alama mbili, naweye utapewa alama mbili”. Alama ya kwanza ilikuwa ikihusu, ya kwamba akikamata mukono wa kuume ya mugonjwa kwenye mukono yake ya kushoto, ugonjwa yake itaonekana kwenye mukono ya ndugu Branham-kwa mfano kansa, uvimbo- na wakati uponyaji inapotendeka, ugonjwa inapotea;alama ya pili ilihusu kupokea ufunuo wa vitu ambavyo hangeliweza kutambuwa juu ya maisha ya mtu ambaye alikuwa akimuombea. Angeweza kusema kwa Jina la Bwana, kila mtu ambaye juu yake alama iliweza kuonekana kwake Kupitia maono: «Umepona kupitia Nguvu za Mungu katika Jina la Yesu Kristo. Bwana Akamwaambia Musa: “Ikiwa hawakuamini, Asema Bwana, na hawasikie sauti ya alama ya kwanza, wataamini kupitia Sauti ya alama ya mwisho”. (Kutoka 4:8)
Kati ya myaka 1946 mpaka 1965, mamia ya watu walipata mazoezi na kushuhudia ya kwamba vipofu walipata kuona, viwete walitembeya, vizuwi walisikia na zaidi wagonjwa wa kansa walipona. Hii ilitokea kwa sababu Malaika wa Bwana alikuwa amesema, wakati wa kazi ya ndugu Branham: “Ikiwa unafikia kiwango watu wanakuamini, sasa hapo hakuna kitu kitakacho shindikana kwa maombi yako, hata pia na kansa. ”
Kulingana na huduma yake, Mwana wa Mungu alikuwa “Nabii” ambae aliye ahidiwa katika Kumbukumbu la torati 18:18, kama vile hiyo inavyo zihirishwa katika Matendo ya Mitume 3:22-23: “Musa alisema: Bwana Mungu wetu Atawainuliya kati ya ndugu zenu Nabii kama mimi; mutamusikiliza katika yote atakayo waambiya, na yeyote yule hatamusikia ataondolewa katika taifa”. Alikuwa akiona katika maono yale ambayo itatokea, anaitamka na ina tendeka, muhusika awe kipofu, mulemavu, mukoma na kazalika.
Hivyo hivyo hiyo huduma moja ilizihirika tena katika wakati yetu: ndugu Branham alikuwa akiona katika maono ile ambayo ingelitendeka, anaitamka na inatokea. Ndiyo sababu mtu wa Mungu alikuwa akisimamia kila mara kwenye kitabu cha Yoana 5:19 na akiitumikisha pia kwa huduma yake: “Yesu akakamata neno, na kuwaambia: kweli, kweli, ninawaambia, Mwana hawezi kufanya kitu kwa Yeye Mwenyewe, Anatenda kulingana na ile Akiona Baba Akitenda: na yote ambayo Baba Anafanya Mwana anayafanya vile vile”.
Kulingana na huduma yake, ndugu Branham alikuwa akilinganisha pia Mwanzo 18, wakati Bwana alipo mutembelea Abrahamu, akisindikizwa na wamalaika wawili na akapana ahadi ya kumuzaa Isaka. Sara ambaye alikuwa katika hema na akiwa akisikiliza akacheka yeye mwenyewe. Bwana Akamugeukia Abrahamu Akamwaambia: “Kwa nini sasa Sara anacheka?” Hivyo hivyo ndugu Branham analinganisha na Yesu, wakati Andrea aliweza kumuongoza ndugu yake kwa Yesu na Yesu sasa akamwaambia: “Wewe ni Simoni, mwana wa Yona”. Kwa Nathanaeli, akasema: “Mbele Filipo hajakuita, ulipokuwa chini ya muzabibu, nilikuona”.
Mwanamke kwenye kisima ambaye kwa yeye Akamufunulia maisha yake ya zamani, akatambuwa: “… ya kama Masia anapashwa kuja (Yule Ambaye Anaitwa Kristo), wakati Atakapo kuja, Atatupasha mambo yote”. Na Masia Akahakikisha: “Mimi ni Yeye, Mimi ninaye kuzungumuzia”. Hii huduma ya kinabii ya kuona mambo kupitia maono na kupokea ufuno ilikuwa ya baraka kubwa kwa wamoja, wakati kwa wengine, kwa kipekee waandishi na wafarisayo, walikuwa wakikwazika na wakimuita Bwana kuwa Belzebuli.
Huduma ikazihirika katika siku zetu, katika wakati huu wa kiunabii ambamo Mwana wa watu alijizihirisha (Luka 17:26-30) tunangoja pia ujio Wake (Luka 17:34-37). Ujio Wake unakuja karibu, kwa siku ile ile, kwa saa ile ile. Hapo wawili watakuwa wakilala katika kitanda moja ao wakitumika katika shamba; mmoja atatwaliwa na mwengine ataachwa. Ile inatendeka kwa muda wakufumba na kufuguwa kwa macho (1 Wakorinto 15: 51-58), kama vile Bwana Alivyo iweka wazi kwetu akiilinganisha na umeme inayo angaa kutokea mashariki mpaka mangaribi (Matayo 24:27; Luka 17:24). Hangeliweza kuyasema waziwazi zaidi ya hiyo. Na tunaamini kama vile imeandikwa. Amen.