BARUA YA MUZUNGUKO Aprili 2012

Ushuhunda wa Kiungu

« »

Kila mara hupatikanaka mambo yasiyo ya kawaida mahali kote ambako Bwana Anapopatikana. Roho wa Mungu Anatenda kila mara katika wakati wa neema: watu waliokolewa, wakafunguliwa na kubarikiwa. Haya yote ilitendeka mara mingi wakati wa huduma ya ndugu Branham. Ilitimia kwa uhakika ile ambayo Bwana Alisema: “Yeye anae amini ndani yangu atafanya pia matendo ninayo yafanya, na atafanya makubwa Zaidi” (Yoane 14:12)

Huyo Mungu Mmoja Aliye jifunuwa Yeye Mwenyewe kama vile Bwana, Yeye kama Malaika wa agano wakati wa biblia, Alijihirisha vile vile katika wakati wetu, katika Nguzo ya moto na katika Wingu la kimbinguni. Bwana Alitimiza ahadi yake: “Dunia haitaniona tena, ila ninyi mutaniona, kwa sababu nitakuwa pamoja nanyi mpaka mwisho wa dunia”. Aliruhusu hata kama kwenye tarehe 24/01/1950, hapo Houston, huko Texas, picha ya Nguzo ya moto juu ya kichwa ya ndugu Branham iweze kupichwa, pia ma picha za wingu ya kimbinguni munamo tarehe 28/02/1963.

Hapo Hustoni, wapigaji picha wa chama cha wapasha habari, Bwana Ayers na bwana Kipamani, moja mukatolika na mwengine muyuda, walikamata ma kartasi zenye hizo picha wakati ya mabishano juu ya uponyaji wa kiungu. Wote wawili walikuwa wapingaji wa ndugu Branham. Wakati wa utengenezaji wa hizo sehemu za hizo picha, ikaonekana kama sehemu zote zilionekana hazina kitu ila picha moja: ile tu ya ndugu Branham pamoja na ile ya mwanga juu ya kichwa chake. Kulingana na ombi la Godoni Laindiseyi, ambaye nilimutambuwa binafsi, sehemu ya negatifu ya hiyo picha ikatumwa kwa mujuzi ambae amefunzwa kuhusu barua ambazo hazieleweke vizuri, kwa Daktari George J. Lasi hapo Washingtoni, ili iweze kuchunguzwa. Nyuma ya kuchunguzwa, tarehe 29/01/1950, akaonyesha barua ya uhakikisho ambayo iliandikwa mara nyingi. Ripoti yake ikawa hivi: mwanga ya kimbinguni ilikuwa, kama sivyo haingeliwezekana ikamatwe picha na chombo cha picha. Hivi, Mungu Mwenyewe Alileta ushuhuda wa uwepo wake na kwa hiyo Alihakikisha neno la mutumishi wake (Isaya 44:26a).

Ni hivyo hivyo kulingana na Wingu la kimaajabu linalo patikana juu ya Flagstaffe kule Arizona, tarehe 28/02/1963. Hapo ndugu alipokuwa akipatikana kwenye mulima Saniseti, yote yakatendeka kama vile alivyo kuwa ameona katika maono. Alinielezeaka hiyo maono munamo mwaka ya 1962 ni kwa sababu alitaka kuhamia huko Tikisoni huko Arizona, kwenye mwezi wa kwanza 1963, akaniomba kuhubiri pa nafasi yake hapo Losanjelosi kwenye mukutano wa wanaume wa baishara wakristu, mukutano ambao Demosi Shakariani alikuwa ametayarisha kwenye kafetariya Kliftoni.

Wingu ilionekana kwenye mbingu wazi ya blu ikaonekana pia nyuma ya dakika 28 jua lilipo lala. Hii ikatokea mahali ambapo ndugu Branham anapatikana wakati alipo pata maagizo kuhusu kuvunjwa ya mihuri saba. Ngurumo saba zenye nguvu zikasikilika na ile eneo yote ikatikiswa kama vile ikitikiswa na mtetemeko ya inchi, mpaka mawe ikaanguka chini ya mulima. Niliona kwa macho yangu hizo lundo za hizo mawe zilizo anguka kwenye mulima huo nilipo safiri kwenda Tikisoni kwenye mulima saniseti.

Kufuatana na ripoti za gazeti, Wingu hiyo ya kimaajabu ilikamatwa picha 80 kwenye mahali mbali mbali. Hata na hiyo gazeti ijulikanayo sana la sayansi lilisafisha picha moja ya tukio hili kwenye ukarasa wa kwanza kwa kuzihirishwa yake munamo tarehe 19/4/1983, hivyo nukuu moja ya Mugaga (DR) James McDonald wa univasti ya Tikisoni, kwenye ukara wa 292 na 294. Gazeti la magazine laife pia likatangaza kupitia picha nyingi kwenye utangazaji wake ya tarehe 17/5/1963. Kufuatana na matamshi ya ndugu Branham, kuliuweko na wamalaika saba wakifanya umbo la piramidi kwenye Wingu hilo na Malaika wa saba kwenye umbo ya wamalaika hao akawaambia neno.

Kuambatana na tukiyo hilo, ndugu Branham anasema hivi: “Mulima ukatikiswa katika eneo fulani kwenye kilomita mingi. Pale kulikuwa wamalaika saba, ambae mmoja alikuwa akishika mpanga mukali mukononi mwake, akaniambia: rudia kwako kwa ajili ya ufunuo wa mihuri saba ambazo zilizo pewa”. Na ile inahusu ile siri ya kweli ya ndoa na talaka, uzao wa nyoka na mambo ingine yote ambayo ndani yazo mulikuwa muvurungano mingi. NI HIVYO ASEMA BWANA” (Muhuri wa pasaka, ya tarehe 10/4/1965).

“Nilikuwa nikisimama, mikono juu nikiomba, wakati mpanga ulipo anguka mukononi mwangu. Munajuwa ile. Nilikuwa nikisimama pale nikiuangalia ilikuwa ni ya kawaida kama tu mukono yangu kwa wakati huo huo. Nilikuwa sijuwe inamaanisha nini. Niliipewa na kwa wakati huo sauti ikasema: hii ni mpanga ya Mfalme. Nyuma ya hapo, wakati Malaika wa Bwana Alipo yafunuwa, ilikuwa ni Neno mukononi mwangu. Hapo hapo baadae, Malaika wa Bwana wakaonekana wakasema juu ya mihuri saba nilipashwa kurudi hapa Jeffersonville na kuhubiri juu mihuri saba” (Siku kuu ya parapanda, 19/7/1964)

Inabidi isemeke tena. Inayo husu ndugu Branham, ilikuwa ni wito na kazi ya kiungu ikisindikizwa na uajibu ya kiajabu, kama ilivyo kuwa kwa Musa. Huduma yake ya kiunabii inapashwa kuwekwa kwenye Neno la kiunabii. Kama vile Paulo alihubiri shauri lote la Mungu, alipokea ufunuo wote wa siri zote na akazieleza; akianza na anguko katika shamba la edeni, mpaka kuingiya ndani ya umilele.

Si vigumu kwa waamini wa kibiblia kuamini kama Malaika alienda kwa Zakaria akimupasha kuzaliwa kwa Yoana mubatizaji ao kama vile alivyo andika katika hiyo kipindi moja ya kwamba Malaika akaenda kwa Maria na kupasha habari za Bwana (Luka 1) ao kama Malaika wa Bwana akaingia kwenye eneo la Petro akiwa anafungwa, akisindikizwa na Wingu kubwa (Matendo ya Mitume 12:7), kama vile Bwana Akatuma Malaika wake kwa Yoane kwenye kisiwa cha Patmosi ili kuwajulisha watumishi wake ile ambayo ingepashwa kutokea upesi, ao pia, ile ambayo inataxwa kwetu katika Danieli 8:15-19, na kazalika.

Je Mungu aliwayi kuuliza wazo la mtu fulani wakati Alimuita Musa, ao nabii mwengine? Ni Yeye Mwenyewe Anaamua kile ambacho Anafanya, kulingana na mupango yake ya wokovu wa milele, ambawo anatimiza katika mwendo ya wakati. Kulikuwa vile katika maisha ya ndugu Branham matukiyo mengi ya kikawaida, ambayo Mungu alimukbalia tangu alipokuwa na myaka saba. Manabii wanatiwa wakfu tangu tumboni mwa mama zao (Yeremia 1:15). Kulingana na Luka 1:15, Yoane mubatizaji akajazwa na Roho Mtakatifu tangu tumbo la mama yake. Paulo pia anashuhudia ya kwamba aliwekwa kando tangu tumbo la mama yake (Wagalatia 1:15).

Kwa huduma yake, ambaye ni mujumbe wa saba kwa wakati wa kizazi cha Laodikia aliingiza kizazi cha bibi arusi. Heri wale wanao jiachiliya kuongozwa katika Neno la kweli, kupitia Roho wa kweli, kama vile Bwana Alivyo waambia waliyo wake: “Roho wa kweli atawaongoza katika kweli yote” (Yoane 16:13). Heri yule ambae hana haja ya kusema: „Ile ingelipaswa kuwa hivi, ao tena namna ingine”, ila anatambuwa ya kwamba itakuwa tu kila mara vile Mungu Aliisema katika Neno lake linalo baki milele! Heri yule mwenye kufikia kuweka Neno kwa nafasi inayo stahili katika biblia yale ambayo ndugu Branham alisema! Hiyo haina maana kwa kutosha matamshi yake yote ambayo ni mengi kwenye nafasi yake na kujilalamikisha: “Nabii alisema: …ǃ Nabii alisema: …ǃ” Neno la Unabii haliruhusu tafsi yeyote ya kipekee (2 Petro 1:20). Kila tafsiri ni uongo, na mtume Yoane anapiga kistari: “… kwa maana hakuna uongo unao toka kwenye kweli” (1 Yoane 2:21). Itakuwa hivyo kila mara: Mahali ambapo kuna ufunuo wa Kiungu, pale hakuna tafsiri, na pale ambapo kuna matafsiri, hapo hakuna ufunuo. Katika kanisa lake la kweli yote inapaswa kuwa ya kibiblia, ni kusema, yenye kuambatana kweli kweli pamoja na agano la kale na agano jipya.

Yote ambayo yalikuwa yakiambatana na huduma ya ndugu Branham yaliweza kutimia. Yale ambayo imehaidiwa kwa kanisa bibi arusi itageuka kuwa kweli ndani yake. Peke yake mambo ambayo ahadi inapatikana katika maandiko matakatifu ile itaweza kutimia “… kwa kuwa, inayo husu maagizo zote za Mungu, ni kwake njo ndiyo, ndiyo sababu tena amina kwa Yeye inatamkwa nasi kwa Utukufu wa Mungu” (2 Wakorinto 1:20). Bibi Arusi wa Mwana kondoo hangoje kamwe nabii mwenye angetokea katika hema muda wa majuma ine huko Amerika. Na hawangojee pia ya kama wafu watafufuka kisha wabaki tena kwenye dunia siku makumi tatu. Bibi arusi anangojea urudishaji wote, kitendo cha mwisho cha Roho Mtakatifu na ujio wa Bwana Arusi wa mbinguni.

Ujumbe wa mwisho ungelipashwa tangulia kurudi kwa Kristo, na hii iko inatimia katika nguvu yake. Wakati wa kipindi cha mwisho wa kitendo cha mwisho cha Mungu, Neno lililo funuliwa litazihika katika wachakuliwa ulimwenguni kote. Kuhusu kuwekwa taji ya kazi ya utkufu na kurudi kwa Bwana na unyakuo: “Tazama, kwamba, yale ambayo tunawaambia kupitia Neno la Bwana: sisi tuliyo hai, tuliyo baki kwa unyakuo wa Bwana, hatutawatanguliya wale waliyo kufa. Kwa maana Bwana Mwenyewe, kwa alama yenye kutolewa, kwa sauti ya Malaika Mukubwa, na kwa sauti ya Malaika Mukubwa, na kwa sauti ya parapanda ya Mungu, Atashuka toka mbinguni, na waliyo kufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. baadae, sisi tulio hai, ambao tutakuwa tumebaki, tutanyakuliwa sote pamoja nawo kwenye mawingu, kwa kukutana na Bwana mawinguni, na hivi tutakuwa na Bwana” (1 Watesalonika 4:15-17). Kunyakuliwa siyo ufunuo wa kipekee; hakika, itatendeka katika kisiri ila ni ukweli mkubwa Zaidi wa nyakati zote: uzihirisho wa wana wa Mungu, kubadiliswa kwa miili yetu, kunyakuliwa yetu na kuingia kwenye chakula ya karamu ya Mwana Kondoo.