BARUA YA MUZUNGUKO Aprili 2012

Malaika wa Agano

« »

Mara ingine tena, ninatumaini kwa mwisho, somo kuhusu Unufunuo sura 11 inabidi iangaziwe kimaandiko. Wakati wa kuja kwake mara ya kwanza, Mungu Akatuma Nabii kwa Taifa lake la Israeli ili kutayarisha njia, kama vile Alivyo iahidi katika Malaki 3:1 (Matayo 11:7-15; Marko 1:1-4). Hii inajulikana kwa ujumla. Katika sehemu ya pili ya hiyo andiko moja ya Malaki 3:1 inayo ambatana na ujio kwa Taifa lake la Israeli, inahusu Malaika wa Agano ambae Atakae ingia katika hema lake: “Na hapo Ataingia katika hema lake Bwana munaye mutafuta pia Mujumbe wa Agano munaye mutaka, tazama, Anakuja, Asema Bwana wa majeshi”. Hii hakika ni HIVI ASEMA BWANA. Hapa haihusu kurudi kwa Kristo Yeye kama vile Bwana wa unyakuo wa Bibi Arusi, ao chakula cha karamu. Hii ujio inaambatana na “Siku ya Bwana”. Andiko Takatifu linatuhakikishia ile: “Ni nani atakae vumilia siku ya kuja kwake? ni nani atakae baki mbele wakati wa kuonekana kwake? Kwa maana atakuwa kama moto wa mufuaji, kama vile potasi ya wafinyanzi. Bwana Ataikala, atayeyusha na kutakasa chuma; atawatakasa wana wa Lawi, Atawamenya kama vile wanavyo menya zahabu na chuma, na watamutolea Bwana zabihu za haki. Hapo sadaka ya Yuda na ya Yerusalemu itakubaliwa kwa Bwana, kama kwa siku za zamani, kama kwa myaka ya zamani. ” (shahiri ya 2-4)

Katika maandiko hayo tunapashwa vile vile ile ambayo itakayo pitika wakati Bwana atakuja kwa Taifa lake la Israeli kama vile Malaika wa Agano. Kwa wakati ule, Atatakasa zabihu za Yuda na za Yerusalemu zitakubaliwa kwake. Ile inatuongoza kwenye utimilifu unao someka. Nyuma ya barua ya mwisho kwa makanisa, katika Ufunuo 3 na arifiyo kali ambayo inapewa kwa waamini: “Yeye ambaye iko na masikiyo asikie kile ambacho Roho Anaambia makanisaǃ” kizazi cha mwisho cha kanisa kinaisha. Ndugu Branham alikuwa akisema mara nyingi: “Kanisa linanyakuliwa kwenye kipindi cha 4 na anarudi katika kipindi cha 19”. Nyuma ya hapo Yoane hamuone tena Mwana wa Mtu akitembeya tena katika vinara saba vya zahabu, ila anamuona Bwana kwenye kiti cha enzi akizungushwa na Upinde: “Na tazama, kulikuwa na kiti cha enzi mbinguni, na kwenye kiti hicho kulikuwa kunakaa mutu. Yule Aliye kuwa Akikaa Alikuwa na kuangaa kama na jiwe ya jaspi na jiwe ya sardwani; na kiti cha enzi kilikuwa kikizungukwa na Upinde…” (Ufunuo 4:2-3).

Katika Ufunuo 10, Bwana Anashuka toka mbinguni kama Malaika wa agano Akizungukwa na Upinde: “Nikaona mwengine malaika mwenye nguvu akishuka toka mbinguni, akizungukwa na Upinde kwenye kichwa chake kuna Upinde, na sura yake kama jua, na miguu yake kama Nguzo za moto” (Ufunuo 10:1. Angaliya yanayo pitika:

  1. Anashika mukononi mwake kitabo ambacho kinafunguliwa kilicho tiwa muhuri katika Kipande cha 5.
  2. Anaweka muguu yake moja kwenye dunia na ingine kwenye bahari na analalamika kwa sauti kubwa kama vile simba akinguruma.
  3. III. Ni hapo sasa nyuma ndipo Ananguruma kama vile simba la kabila la Yuda (Mwanzo 49:9) ambapo sauti za ngurumo saba zinasikika.

Tangu wakati ambapo anaapa kama Malaika wa Agano, kungali tena myaka tatu na nusu mpaka mwisho wa ziki na mwanzo wa utawala: “… na akaapa kwa Yeye Anae ishi milele ya kwamba itakuwa kwa wakati moja, kwa nyakati, na kwa nusu ya nyakati, na ya kwamba vitu vyote hivyo vitaisha wakati nguvu ya Taifa takatifu itavunjwa kwa lote” (Danieli 12:7b). Ni HIVI ASEMA BWANA ndani ya Neno lake.

Sasa Anapo nguruma kama simba, hii ujio pia inaangaziwa na mistari tatu ya maandiko. La kwanza ni Yeremiya 25:30-36: Bwana ananguruma toka juu, kwenye makao yake takatifu, Atasikilizisha sauti yake, Atanguruma kwenye eneo ya makao yake; atatowa sauti kama vile wenye kukanyaga chombo cha kusaga, juu ya wakaaji wote wa dunia. Habari inafika mpaka mwisho wa dunia; kwa sababu Bwana anabishana pamoja na mataifa. Anaingia hukumuni juu ya mwili wote, anawaweka waasi wote kwenye mpanga wa zamani, Asema Bwana (ona pia Isaya 63:1-6 na Ufunuo 14:14-20).

Andiko ya pili Hosea 11:10: “Watamufwata Bwana, Ambae atanguruma kama simba, na wana watakimbilia baharini”.

Andiko la tatuni Yoeli 3:15-16: “Jua na mwezi vitatiwa giza, na nyota zitaondowa mwanga wao. Toka sayuni Bwana Ananguruma, toka Yerusalema sauti yake inasikika, mbingu na dunia vinatikiswa. Lakini Bwana ni makimbilio kwa Taifa lake, maficho kwa wana wa Israeli”.

Tarehe 17/03/1963, ndugu Branham alisoma kwa sauti kubwa andiko katika kitabo cha Ufunuo 10 na nyuma, analinganisha na maandiko ambayo tumetaja hapo juu, Alisema: “Ikiwa mulitambuwa: ni Kristo: katika agano la kale, Anaitwa “Malaika wa Agano. Anakuja sasa hapo hapo kwa Wayuda, kwa kuwa kanisa limekamilika”. Ni kweli. Halikamilishwe tu, ila pia linanyakuliwa.

Hapa tunamuona Bwana kama Malaika Mukubwa wa Agano Akifunikwa na Wingu. Ni hiyo Wingu moja iliyo kuwa ikisindikiza Taifa la Israeli – Bwana Yule Mmoja, Malaika Yule Mmoja wa Agano. Upinde kwenye kichwa chake inashuhudia Agano lile Alilo fanya na Israeli. Kwa hivyo, Ananguruma kutoka mulima Sioni, wa Yerusalemu. HIVI ASEMA BWANA ndani ya Neno lake. Kila kitu kingine chochote ni tafsiri tu ya kimawazo (2Petro 1:20). Yeye ambae haamini kweli ya Neno amehukumiwa kuamini uongo. Bwana anaweza tu kumuzungumuzia yule ambae anaheshimu kabisa Neno la Mungu. Yeye anaye weka kwenye nafasi nzuri kwenye biblia ile ambayo ndugu Branham alisema, anaamini kama vile maandiko inavyo sema. Amen. Ni hivyo ndivyo tuko Bibi Arusi Neno. Mafundisho ingine yote kuhusu Ngurumo haziko za kibiblia, kwa sababu haziwezi kupatikana ndani ya biblia na hakuna hata ushuhuda moja yenye kutolewa kuhusu hiyo katika maandiko. Ole kwa yule mwenye kuongeza jambo fulani kwenye ushuhuda inayo eneya tena yenye haki ya maandiko matakatifuǃ (Ufunuo 22).

Kulingana na Malaki 3:1b-5, Bwana Anaingia kwenye hekalu lake kwa muda huo. Ni wakati ambayo “mupinga Kristo”, kama “mwana wa upotevu” na adui wa Kristo, anajiinuwa juu ya yote katika kiburi yake, ataenda kuikala katika hekalu. Bwana Atamumaliza nguvu kwa pumzi ya kinywa chake (2 Watesalonika 2).

Katika Ezekieli, kipande cha 40 mpaka 47, hekalu inatuonyeshwa, pia na muto, unao shuka tangu hekalu ukielekea kwenye Agedi mpaka bahari ya mauti. “Akanibeba kwenye mulango wa nyumba. na tazama, maji ilikuwa ikitoka kwenye kiti cha nyumbani, kwa mashariki…” Katika Zakaria 14:20-21, imeandikwa ya kwamba hata na vyombo vya kuchamusha vitawekewa wakfu ndani ya nyumba ya Bwana. Katika Isaya 66:6 tunasoma: sauti yenye kusikika sana inatokea katika muji: “Sauti inatokea kwenye muji. Ni sauti ya Bwana, inayo lipa maadui zake mushahara yao”.

Katika Ufunuo 11, imetajwa huduma ile ya mashaidi wawili. Tangu shahiri ya kwanza imeandikwa: “Simama, na upime hekalu la Mungu, mazabahu na wenye kuiabudia” Kwa wakati ule, hekalu lililo bomolewa kwenye mwaka wa 70 nyuma ya Kristo litajengwa tena.

Wayuda wenye kuombea kwenye ukuta wa maombolezo kila mara wanamaliza maombi yao kwa maneno haya: “Elohim Adonai, fanya ili hekalu liwezwe kujengwa tena na Masia Aweze kuja”. Hapo hapo nyuma, kwenye shahiri la 2, imeandikwa ya kwamba kwa wakati ule, “Muji Mutakatifu” – kila mara ni Yerusalemu – utakanyagwa kwa miguu ya wamataifa myezi 42, ni kusema myaka tatu na nusu. Katika Ufunuo 13:3, imesemeka ya kama wale washuhuda wawili watatabiri muda wa masiku 1260, inayo fanya pia kwa ujumla myaka tatu na nusu. Kwa kuepuka ili tusifikie kumaliza ya kwamba inahusu ile ile myaka tatu na nusu, nyakati ziliwekwa mara moja kwa wakati moja ya masiku 1260, kulingana na huduma ya wale manabii wawili na ingine wakati kwa myezi 42, ambayo kwa hiyo muji utaweza kukanyagwa. Wakati wa myaka tatu na nusu za kwanza, wale washuhuda wawili wanatimiza huduma yao. Wakati wa myaka tatu na nusu zinazo fuata itatendeka ile ziki kubwa, ambapo ziki ya waamini waliyo baki itafanyika na zaidi wayahudi: “Na akapewa uwezo ya kutenda muda wa myezi 42”. Nyuma ya hiyo myaka tatu na nusu juu ya Israeli, utawala utatangazwa. Ni HIVI ASEMA BWANA katika Neno lake “… na watakatifu watatolewa kwenye mikono yake kwa muda, nyakati, na nusu ya nyakati. Baadae hukumu… Utawala, uwezo, na ukubwa wa mafalme zote ambazo ziko chini ya mbingu, zitapewa kwa taifa ya watakatifu ya Aliye juu. Utawala Yake ni utawala ya milele, na watawala wote watamutumikia na kumutii” (Danieli 7:25-27).

Kama vile Alivyo yafunuwa kwa ukweli kwa watumishi wake manabii (Amosi 3:7), imetuambiliwa katika Ufunuo 10:7, ya kwamba wakati Malaika wa saba atapiga parapanda yake (shofar), Siri ya Mungu itatimizwa. Kristo, Mupakaliwa, Mkombozi, Ndiye siri ya Mungu iliyo funuliwa (1Timoteo 3:16). Wayuda hapo zamani hawa kumutambuwa, ila sasa watamuona, Yule Ambae walimusulubisha (Zakaria 12:9-14). Katika Ufunuo 11:15, tunapata utimilifu: “Ufalme wa dunia umetolewa kwa Bwana wetu na kwa Kristo wake; na Atatawala milele na milele. Haiwezi kuwa eti ni kwa namna moja ao eti labda ni kwa namna ingine, kwa sababu Neno la Mungu kila mara ni “Ndiyo na Amina” tena kwa kila somo.

“Nitafanya nawo Agano la salama, na kutakuwa Agano la salama pamoja nawo, nitawaweka, nitawazidisha, na nitaweka fasi yangu ya Utakatifu kati yao kwa milele. Makao yangu itakuwa kati yao; nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa Taifa langu. Na mataifa watajuwa ya kama Mimi ni Bwana, Anae takasa Israeli, wakati nafasi yangu ya Utakatifu itakuwa kwa siku zote miongoni mwao” (Ezekieli 37:26-28). Na itakuwa kama vile maandiko yote ya biblia inavyo shuhudia.

Tuiseme tena mara ingine: ile mihuri ine ya kwanza inaambatana na nguvu ya mupinga kristo katika hali zote ine za hiyo mihuri ine (Ufunuo 6:1-8) ikienda sawasawa na vizazi vya kanisa (Ufunuo 2+3) muhuri ya tano unaonesha wayuda waliyo kufia Injili – wale pia kwenye mazabahu – chini ya mazabahu ikisemeka ya kama kizazi italipishwa kisasi damu yaoya na ya mabaki ya marafiki na ndugu zao watasumbuka kupitia kifo kama wao (Ufunuo 6:9-11).

Katika muhuri wa sita, tunaona kiingiliyo katika siku ya Bwana: tetemeko mukubwa la dunia inafanyika, jua inatiwa giza, mbaramwezi inageuka kama damu, nyota zinaanguka toka mbinguni na imeandikwa kweli: “… kwa maana siku kubwa Yake ya gazabu imefika, ni nani anaye weza kusimama?” (Ufunuo 6:12-17). Tangu sasa kila mmoja ni sherti ataelewa ya kwamba matukiyo ambayo inatajwa itapitikanaka nyuma ya unyakuo, kwa wakati wa muhuri wa sita na wa saba. Tarumbeta zote za hukumu, pia vikombe saba vya gazabu viko pamoja kwenye muda huo (kipindi cha 16). Kunabaki tu sasa hukumu ya babeli mukubwa, ambae anavaa mavazi yenye kuangaa (kipindi cha 17+18).

Hakuna hata mmoja anaye kuwa sehemu ya Bibi Arusi ambae iko na haja ya kujiusisha na yale ambayo itapitika kwenye dunia kwa wakati ule. Yote itatendeka kama vile imeandikwa, kipindi kwa kipindi, shahiri kwa shahiri. Muhuri wa saba (Ufunuo 8:1) haina tu ile kimya katika mbingu. Tangu shahiri ya pili imetajwa kwetu ile sasa ambayo inatendeka: Yoane akawaona wale malaika saba ambawo wanapatikana mbele ya Mungu, wakipewa parapanda saba. Na tunatambuwa pia ni pigo gani inayo pata dunia kwa kila sauti ya kila parapanda. Amen. Kwa sehemu ya mwisho, yote yanasemeka kwa namna ya uhakika, yenye kuhusu kipindi cha 7, kipindi cha 8, 9, 10, 11 ao tena mbali zaidi. Yote yatatendeka hapa duniani.