BARUA YA MUZUNGUKO Aprili 2012
Kwa heshima kubwa na kujazwa na shukrani, tunatambuwa ile ambayo Mungu Alifanya kwa namna ya kimaajabu kwa wakati wetu. Kwa namna Alitaka kutuonyesha njia, kuturudisha kwenye mwanzo, kwenye musingi wa asili, kwa mafundisho ya wamitume, kwa yakini ya uhakika ya Neno lake, kwa kuwa ni kwa namna hiyo tungeweza fanya mazoezi ya umoja wa kweli, pia na ukamilifu kwa neema yake.
Jambo la muhimu zaidi kuhusu hao waevanjilisti waine ilikuwa kwamba yote yaliyo pitikana, tangu Matayo 1 mpaka Yoane 21, iweze kuwekwa sawasawa na andiko: “Hayo yote yalifika ili itimie yote Bwana Aliyo tangaza…” (Matayo 1:22a). “Mambo haya yote yalitokea, ili andiko litimie… (Yoane 19:36a) Petro alifanya hivyo hivyo, kwanza mbele ya siku ya pentekoste: “Na, imeandikwa katika kitabu cha zaburi…” (Matendo ya Mitume 1) na zaidi nyuma ya Roho Mtakatifu kushuka: “Lakini ni hii hapa iliyo semwa na nabii Yoeli…” (Matendo ya Mitume 2). Nyuma ya ufufuko, Bwana wetu Anasema: “Hiyo ndiyo niliyo waambia wakati nilipokuwa pamoja nanyi, ya kwamba ilibidi itimizwe yote iliyo andikwa juu yangu katika sheria ya Musa, katika manabii, na katika zaburi” (Luka 24:44). Kwa hiyo, ni kulingana na utimilifu ndiyo sababu Akapana ufahamu wa maandiko kwa waliyo wake (shahiri ya 45).
Paulo pia akarudilia mara nyingi maandiko matakatifu na akatambuwa kuweka vizuri huduma yake kwenye Isaya 49:6, wakati wokovu ulipita kwenye wayuda kwenda kwa mataifa: “Kwa maana hivyo ndivyo tulivyo amuriwa na Bwana: nilikuweka ili ukuwe nuru ya wamataifa, kwa kubeba wokovu mpaka mwisho wa dunia” (Matendo ya Mitume 13:41-51). Akawekwa kando “ili atangaze Injili ya Mungu, iliyo ahidiwa tangu zamani kwa upande wa Mungu kupitia manabii wake katika maandiko matakatifu” (Waroma 1:1-5). Hivyo, tunaweza kuweka huduma ya ndugu Branham katika maandiko matakatifu. Biblia ndio musingi pia wa pekee wa mahubiri yangu. Ninapashwa kujilinganisha na Matayo 24:45-47, kwa sababu Bwana Yeye Mwenyewe Aliniiambia kwa sauti kubwa. Ninaweza kujilinganisha na 2 Timoteo 4:1-5, kwa sababu Bwana Aliniamuru kwa sauti ya nguvu. Huduma ya sasa inabidi iwekwe pia kimaandiko.
Ile haina maana kuwa munyofu na kusema kuhusu ndugu Branham na kuhusu huduma yake. Jambo ambalo ni muhimu sana ni kuweka vizuri na kwa namna ya kimaandiko Neno lililo andikwa na lililo funuliwa. Hiyo inahusu kwa mfano, kutochanga Ufunuo wa mihuri saba ambayo ilitendeka kwa mwaka wa 1963 pamoja na utimilifu ya zile mihuri tena bila kuichanga pamoja na kurudi kwa Kristo. Kuonekana kwa Wingu ilikuwa tu ni alama kwa ajili ya kuvunjwa ya mihuri. Ndugu Branham aliyasema wazi wazi. Matukiyo yatakayo kuja ilitangaziwa kama vile imekuja kutimia. Ni hivyo pamoja na manabii wote wa kimaandiko. Kwenye kipindi cha 53, Isaya akaona kusulubiswa kama vile imekwisha kutimia, ijapo hivyo kulikuwa kunabaki myaka 800 huko mbele. Mutume Yoane akaona mambo hayo yote ambayo ilibidi itokee, kama vile ilikwisha kutimia. Akaona karamu ya Mwana Kondoo (kipindi cha 19), na kwa kipindi cha 20 akaona hukumu mbele ya kiti cheupe hata na Yerusalema mupya ikishuka toka mbinguni, ila hii ikiwa ingali mbinguni. Akaona pia mbingu mupya na dunia mupya (kipindi cha 21).
Tungali kwenye wakati wa neema; inabidi ile isemeke tena waziwazi. Damu ya Agano jipya ingali kwenye kiti cha neema. Yesu Kristo Ndie Mupatanishi wa agano jipya na anabaki Mutetezi wetu mpaka muchaguliwa wa mwisho aitwe (Waebrania 9:11-22 na zingine). Kwa kila kizazi cha makanisa, Mukombozi Alikuwa tu Akidai haki yake kwa wagombolewa wake. Atakamilisha madai yake wakati wa kuja kwake kwa kugeuzwa ya miili yetu. “Na si Yeye Mwenyewe; si Yeye pekee, ila na sisi pia, ambawo tuko na arabuni ya Roho, nasi pia tunauguwa ndani yetu, tukingoja kuwa wana, na ukombozi wa miili yetu” (Waroma 8:23). Kulingana na Ufunuo 7, kundi ambalo linavaa ma kanzu mweupe linapashwa pita kwanza kwenye ziki kubwa, kwa kuwa lilisafishwa katika damu ya Mwana Kondoo (shahiri ya 14). Heri yule ambae anaamini kama vile andiko inavyo sema na kujitenga na tafsiriǃ
Tangu myaka mingi hatukuacha kutangaza kibiblia huduma ya kimaajabu ya ndugu Branham, kwa kuiweka kwa uhakika kwenye musingi wa maandiko matakatifu. Ni yenye wazi ya kama alikuwa mujumbe wa kizazi cha mwisho cha nyakati saba za makanisa, kwa huduma hiyo siri zilifunuliwa na mafundisho yote, hakika yote yamewekwa katika nafasi yake ya asili, kama vile hapo ku mwanzo. Tunajuwa pia ya kwamba alikuwa akingojea zaidi, ya yale ambayo yalikuwa imekwisha kutimia. Nani anaweza kuyatambuwa vizuri kama mimi ambae ninatafsiri mahubiri zake kwenye kijermani tangu mwaka wa 1958? Wakati tarehe 28/11/1963, ndugu Branham alisema kwamba kanda zake za asumaku zinasikika na kutafsiriwa katika kijermani mbele ya mamia ya watu, hangeweza kutaja mtu mwengine, kwa maana ni mimi tu njo nilikuwa nikifanya ile kwa wakati ule.
Je shabaa ni kwamba matamshi yote ya ndugu Branham iweze kuwekwa kama vile yakini juu ya maandiko, kama vile kwa huzuni wamoja wanapo fanya, ukiona wakitumikisha matamshi yake kwa kushuhudia mafundisho yao wenyewe? Je historia hairudie kulingana na yale Petro aliandika zamani, ni kusema ya kama wale ambawo hawasimame vizuri katika Neno waaribishe maana ya mambo magumu kwa kuelewa kwa ajili ya uharibifu wao wenyewe? (2 Petro 3:14-18) mara nyingi matamshi yake inatamkwa kwa unyofu wote, ila sasa, bila kuweka kwa nafasi inayofaa katika maandika matakatifu. Kwa hivi, unaweza kuwa munyofu, na ukiwa ndani ya kosa kwa unyofu wote, ukipendaa kufanyia Mungu kazi pasipo kuitwa kwa kuifanya, na kwa hiyo pasipo kuwa katika mapenzi yake.
Wito na kazi ya Kiungu ambayo Bwana Alihakikisha tarehe 03/12/1962, mbele ya washuhuda hao Sothman na Woods, siyo ya kutupiliwa. Huduma yangu inaambatana na huduma ya ndugu Branham katika mupango ya wokovu ya Kiungu. Kwa jibu la maongezi mamoja inayo jengwa kwenye matamshi ya kipekee ndani ya makundi ya ujumbe ya wakati wa mwisho, inabidi isemeke mara ingine: Ikiwa hakuna ahadi kwa jambo fulani ndani ya biblia, ni kusema na hakuna utimilifu. Matafsiri inajaa roho za uongo, na hatuna na lazima yake, kwa sababu hiyo inaleta kwenye kuhayarika. Huduma ya ndugu Branham ilikamilika hakika, kama vile huduma ya Musa, ya Eliya na Yoane mubatizaji hata naingine huduma yeyote, kwa sasa kwa kufanya kazi pamoja na watumishi wengine katika ulimwenu wote. Ila kama vile ndugu Branham alivyo yasema mara nyingi, hii ingelipaswa kwanza kuwekwa kwenye gala. Ninaweza kushuhudia ya kama niliweza fanya yote mawili, kufuatana na agizo la Bwana: ya kwanza kuweka katika gala na baadae kugawa. Tangu mbele haikusemwa kwamba kulingana na Neno, “Kweli ninawaambia, atamuweka juu ya vitu vyake vyote” (shahiri ya 47) “Leo andiko hili limetimia”. Ujumbe ya mwisho inaambatana hapo hapo na Matayo 25: “Tazama Bwana Arusi, mwende kumulakiǃ”. Wabikira safi wanangojea ile, wanasafisha taa zao na wanajaza vyombo vyao. Wapumbafu wanapita pembeni ya hayo na hivyo wanakosa matayarisho yao. Yeye anae kataa huduma iliyo fuata inabidi ajiulize ikiwa kweli alielewa huduma iliyo tanguliya. Itakuwa namna gani ikiwa Bwana hakuweza shurulikia Yeye Mwenyewe, myaka kwa kuanza, ili kwa mwisho nyuma ya kwenda kwa mujumbe, ujumbe iweze kabisa kuletwa katika ulimwengu wote?