BARUA YA MUZUNGUKO Aprili 2012
Sasa, tayari mbele ya kurudi kwa Bwana wetu, ni ya muhimu ya kwamba wale wanao fanya sehemu ya Bibi Arusi wa Yesu Kristo waweze kutoka katika utumwa na katika muchafuko ya kiroho, na hii ni katika muzunguko ya Ujumbe, ili waweze kumutumikia Bwana kweli kweli kama vile Taifa Lake lililo gombolewa. Tazama ujumbe pekee wa kibiblia inayoita kwa kutoka: Murudie kwenye mwanzoǃ Murudllie Nenoǃ Kurudlilia Injili ambayo Paulo na Mitume waliyo hubiri. Ingine utangazaji yote ni laana, kulingana na Wagalatia 1:6-10. Kila moja angelipashwa soma kipindi hiki na kuyakamata kwa makini, pia vile 2 Wakorinto 11:1-6. Paulo alitaka kumuonyesha Kristo bikira safi. Ndugu Branham aliitamani vile vile. Kila mutumishi wa kweli wa Kristo anayatamani. Ila, kama vile nyoka tangu mwanzo aliwashawishi wote ambawo hawakusimama imara katika Neno, pia tena mpaka kwa siku hii, adui anaendelesha kazi yake. Shetani anabaki kila mara kwenye somo, ila hapana ndani ya kweli (Yoane 8:44).
Kwa hiyo, wachaguliwa wa kweli, wale ambawo ni sehemu ya Bwana Arusi hawawezi kudanganywa. Kulingana na Waefeso 5:27, ni Bwana Mwenyewe Atakaye leta mbele Yake kanisa lake lenye utukufu, bila taka taka ao kikunjo. Ni ya muhimu tuamini na kufanya mazoezi ya ma ahadi ambazo Bwana Alifanya kwa wakati wetu. Ndugu Branham alikuwa akisema: “Inasemeka nini katika Malaki 4:5? Ni urudishaji, urudishaji katika Imani ya asili ya pentekoste, kwa watu wakiwa na ujumbe moja ya kipentekoste, kwenye ushuhuda moja wa pentekoste, kwenye Mungu Moja, kwa nguvu moja, kwenye mafundisho moja na yote sawasawa, jambo moja, pamoja na uzihirisho moja ya ile Nguzo ya moto iliyo mutokea Paulo na ikamwangusha chini kwenye njia ya Damasi, ikiwa kati yetu leo ikifanya kitu kile kimoja kama vile zamani. ” (Wakati na alama ya muungano, ya tarehe 18/08/1963)
Liko wapi kanisa ambalo limeitwa kwa kutoka sasa? Tunaona pale mpaka Musa alikuckuwa kusanyiko la Israeli kupitia uongozi wa Mungu wa hapo hapo. Nyuma ya hapo, nabii alitimiza kazi yake. Ile inatupatia nguvu ya kusoma maneno yake katika kitabu cha Kumbukumbu kwenye kipindi cha 27, kwenye kipindi cha 34, vipindi ambavyo viko ndani somo zote, kwa kipekee baraka zote za kabila 12. Musa akapanda juu ya mulima wa Nebo ili aweze kuiona inchi iliyo ahidiwa, lakini haikuruhusiwa kwake kuingia. Ni hapo Bwana Alimuchukuwa mutumishi wake, akiweka mwisho kwa wakati moja ili kuanza ingine … kwa uongozi wa Yoshua, makuhani wakachukuwa sandugu la Agano na kama vile bahari nyekundu kule nyuma, Yordani pia ikavukwa ikikauka kwa miguu na wakariti inchi iliyo ahidiwa. Vipindi katika kitabu cha Yoshua vinashuhudia pia historia ya wokovu ya Kiungu. Katika kitabu hiki tunasoma vile namna gani ile iliendelea: “Yoshua akaliambia taifa: mujitakase, kwakuwa kesho Bwana Atafanya maajabu katikati yenu. Na Yoshua akawaambia makuhani: Mubebe sandugu la Agano, na mupite mbele ya Taifa” (Yoshua 3:5-6). Hatuna lazima ya nabii wa munane. Ile ambayo tunahitaji ni Neno la Agano, maandiko matakatifu. Amen.
Nyuma Bwana Mwenyewe mpaka hapo Akisha kusindikiza Taifa lake la Israeli, Akaonekana sasa mbele ya Yoshua sawa vile Kiongozi wa Jeshi la Bwana, mpanga ikiwa uchi mkononi mwake. Yoshua akaanguka mpaka uso chini kwa kumwabudu na kumuomba: “Bwana Anasema nini kwa mutumishi wake? Na Kiongozi wa Jeshi la Bwana Akamwaambia Yoshua: ondowa viato vyako kwenye miguu yako, kwa maana nafasi ambayo unasimama ni takatifu” (Yoshua 5:13-15)
Nyuma kukakuja siku ya kipekee, siku ya ushindi kwa Taifa la Mungu. Jua likasimama katika mbingu na Kiongozi wa Jeshi la Bwana Yeye Mwenyewe Akakaribia na kupigana kwa ajili ya Israeli. Ila, je tunaona ni mpaka wapi kanisa limeongozwa na huduma ya ndugu Branham? Tunaona vile ile iliendelea na inaendelea tena mpaka kwa siku hii?
Hii kitabu iweze kuwa musaada kwa kuongonza wale wote ambawo ni sehemu ya kanisa Bibi Arusi kwa kusikia Sauti ya Bwana Arusi wa mbinguni na waweze kujiachilia kuingia katika mapenzi na mpango wa Mungu. Katika urudishaji kamili ambayo tumehahidiwa, kanisa la Bwana, litakuwa sawasawa vile ku mwanzo kama Mwili wa Kristo, nyumba ya Mungu, Nguzo na musimamo wa kweli, likiwa na ile mahubiri moja, mafundisho moja, ile ubatizo moja ya maji, ubatizo moja ya Roho Mtakatifu. Yote kama ilivyo kuwa hapo ku mwanzo: kuelewa Bwana Mmoja, imani moja, ubatizo moja (Waefeso 4). Hapana kundi moja hapa na kundi lingine pale, lakini kama vile waamini wa zamani ambawo walikuwa roho moja na nafsi, ndivyo watakuwa tena kwa mwisho, roho na nafsi moja, katika kila inchi na katika kila muji.
Tuna uhakika. Bwana Mwenyewe, Mushindaji wa Golgota ambae Alishinda juu ya nguvu zote za adui, akamuweka hazarani, Yeye Anatembea mbele yetu (Wakolosai 2:12-15). Yeye Ambae alituleta kwa Mkono wake wa nguvu, atatuingiza pia kwa Kuume yake inayo inuka. “Kuume ya Bwana inainukaǃ Kuume ya Bwana inazihirisha Nguvu Zakeǃ” (Zaburi 118:15-16). Hakuna ahadi itakayo baki pasipo kutimilika. Bwana wetu Yeye Mwenyewe na Mwokozi iko anamaliza kazi yake na tulipewa uwajibu ya kushiriki ile.