BARUA YA MUZUNGUKO Aprili 2012
Ninaweza kuangalia nyuma kwa zaidi ya myaka makumi sita katika Ufalme wa Mungu. Ni kwa mwaka wa 1948 niliweza kumugeukia Kristo na nikapokea uhakikisho ya kuwa mwana wa Mungu. Pamoja na mazoezi zingine ambazo Bwana Mwaminifu Alinijaliya, ninaendelesha mwendo pamoja na Yesu Kristo. Kwa mwaka wa 1949 nikapata sehemu kwenye mukutano wa kipentekoste wa ulimwengu wote katika mji wa Hamburg. Nilianza kuhubiri kila mara tangu mwaka wa 1952.
Mazoezi kwenye mikutano na kukutana mara nyingi na ndugu Branham katika myaka ya 1955, 1958 na 1962 iilikuwa ni vipindi vya maana kwa maisha yangu ya kiroho. Ningali na baruwa 21 zikishuhudia ushhirikiano wa palepale pamoja na yeye. Tarehe ya kwanza ya 11/11/1958 ndiyo ya mwisho, na tarehe 30/09/1965. Kupitia mahubiri yake ambayo ilitumwa kwangu mara kwa mara, niliongozwa kila siku kwa kilindi ndani ya maandiko matakatifu.
Munajuwa ninyi nyote tangu myaka mingi maneno ambayo ilitamkwa wakati wa kuitwa kwangu, tarehe 02/4/1962. Mbele nilikuwa nikihubiri Neno, lakini nyuma ya siku ile, nilipanga kwenda katika miji ingine. Kwa musingi wa kazi hiyo, nilienda muji kwa muji, inchi kwa inchi na kontinenti kwa ingine kwa kuhubiri Neno, kama vile Bwana Alivyo niamuru.
Kwa wale wote ambawo wanaweza kuiamini, ninashuhudia mara ingine kwa ukweli wa mazoezi niliyoishi ambayo nilizungumuzia, sawa vile nilimuona ndugu Branham wakati ya kufa kwake, siku ya tano tarehe 24/12/1965, akiwa akipanda mbinguni kwenye mawingu ikifanana na ile ya tarehe 28/02/1963. Hii nayo pia ni kweli kama vile mungu anavyoishi. Elisha nae akaona vile eliya alivyo nyakuliwa mbinguni (2 wafalme 2). Kwenye maono hiyo nikasema: “Ndugu Branham wewe hauko hata Mwana wa Mtu, ni nini sasa ninakuona kwenye mawingu?” Kwa wakati ule, sikujuwa bado kuhusu ajali ya gari aliyo ipata tarehe 18/12/1965.
Macho yangu yalikuwa hakika ya mwisho kuona ndugu Branham ndani ya sandugu, mbele ya kiongozi wa mazishi, bwana Kuti, tarehe 10/04/1966. Sura yake ambayo ilikuwa imepata majeraha kali wakati wa ajali alikuwa akionekana amepata umbo kamili na alikuwa ametiwa dawa ya kuto oza. Alikuwa akipendeza kwa kuona na alikuwa na ka kicheko ka kawaida.
Mazishi ikafanyika siku ya juma pili ya pasaka ya tarehe 11/04/1966. Kungojea kuona ufufuko yake itendeke ilikuwa kubwa. Ndiyo sababu maziko ikakawiya juu ya wahuzuriaji ambawo walikuwa wakiimba bila kuacha nyimbo hizi: “Amini tu” na “ Juu ya mabawa ya Huwa mweupe kama teluji”.
Mangaribi ya siku hiyo nyuma ya majeshi, nikaelewa ya kama wakati ilikuwa imefika ya kubeba ujumbe ambawo Mungu Alipana katika ulimwengu wote. Kama vile ndugu Branham alivyo niambia tarehe 03/12/1962, nilikuwa nimengoja kwanza mbele ya kugawa chakula cha kiroho, mpaka nipokee inayo baki na wakati ipate kutimia. Kufuatana na mahubiri ya kiungu, ningeliweza tangu sasa hapo kutimiza kazi yangu kwenye mupango ya wokovu.
Ni hivyo kwa myaka ya 1966/1967, nikaanza kufanya na kuleta mikutano katika miji 25 ya Ulaya ya mashariki. Nikaalika pia reverandi Piri Grini kwa hiyo mikutano. Tangu mwaka wa 1968, nlianza kusafiri pia katika inchi za Ulaya ya mashariki, ukitia na Rusia. Nyuma inchi zingine zikafuata na kontinenti zingine. Kulingana na aliko nyingi, nikahubiri vile huko Kanada na Amerika, kisha pia kule Amerika ya kilatini, huko Afrika, huko Asia na mpaka kule Australia na kule Zelandi mupya. Mupaka mwaka wa 1979, nilihubiri na kutangaza ujumbe wa wakati wa mwisho, Neno la Mungu ambalo ni la kweli milele katika mataifa 85, kwa kupanda Neno kama vile mbegu ya asili, vile Bwana Mwenyewe alivyo yafanya (Matayo 13:37-38; Marko 4:14; Luka 8:11). Ilikuwa myaka iliyo barikiwa zaidi kwa kazi yangu kwa Bwana. Mungu Mwaminifu Alipana Neema yake na baraka zake kwa kila safari.
Kwa muda wa hiyo myaka yote, tuliishi pia hapa Krefeldi mikutano tu iliyo barikiwa, katika uwepo wa Mungu na wakati ambamo Kitendo cha nguvu cha Roho kilijizihirisha. Ila kwenye mwezi wa tano mwaka wa 1979, shetani akataka kunibomowa pia na kusanyiko pamoja na kazi, kwa hiyo Neno ambalo Bwana Alilo sema kuhusu Kanisa lake lilizihirika kama kweli “… na milango ya kuzimu haitaweza kulitikisa” (Matayo 16:18b). Niliweza kufanya mazoezi mimi mwenyewe ile ambayo Alimwaambia Petro: “Simoni, Simoni, shetani alikutaka ili akutikise kama ngano. Lakini nilikuombeya kusudi Imani yako isiregee; nawe wakati utakapo okoka, uwatiye ndugu zako nguvu” (Luka 22:31-32)
Leo, ninaangaliya kwa hiyo myaka yote nyuma na hesabu ya inchi ambazo zime tembelewa zimetimia inchi 85 – 155 kufikia mwaka wa 1979. Niliwahi kutangaza Neno la damani lililo funuliwa ijapokuwa mazarau na kunisemea uongo. Kwa sasa, maelfu wanasikiya Neno la Mungu kupitiya stesheni za ma televisheni ambazo zinatangazwa kila juma katika sehemu zote za ulimwengu. Ulimwengu muzima iko inafikiwa. Mahali ambapo si vyepesi kufika mimi mwenyewe, sasa ni kurudilia mahubiri kwenye radio na kwenye televisheni, tena kupitia mutandao, kupitiya vitabu na kwa zaidi ya tepe 7500 ambazo zinatumwa kila mwezi zikiwa katika luga 13 tofauti. Neno hili linatimia: “Habari njema hii ya Ufalme wa Mungu itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote…” Na kwa wakati moja Bwana Anaita wachaguliwa wake kutoka katika kila muchafuko ya kiroho.
Kwa mwisho, tunangoja urudishaji mara mbili, kwa Kitendo cha nguvu cha Roho wa Mungu, kukiwa vile vile kwa uhakika kujazwa na upendo wa Kiungu. Upendo kamili peke yake ndio unaweza kuingia kule juu na ni upendo wa Mungu ambao umemwanga ndani ya roho zetu kwa Roho Mtakatifu. Ni hapo sasa ndizo karama kenda za Roho (1 Wakorinto 12+14) zitazihirika kwa ukamilifu wa kanisa, na pia hizo matunda kenda ya Roho katika maisha ya kila moja (Wagalatia 5:22-24). Upendo wa Mungu, kama vile ilivyo zihirika kwenye musalaba wa Golgota, inaunga kati yao wote wachaguliwa na ni kila mara kupitia usamehe na upatanisho. Kifungo cha ukamilifu siyo ujuzi wa kipekee, bali ni upendo wa Mungu ndio una wakamata wachaguliwa wote. Paula analeta neno hili kwa wachaguliwa na ndani yao linageuka kuwa uhakika: “Hivi sasa, kama vile wateule wa Mungu, watakatifu tena wapendwa, muvae upendo ya rehema, uwema, unyenyekevu, upole, uvumilivu. Muvumuliane ninyi kwa ninyi, na ikiwa, moja ana cha kushitaki mwengine, musameheane moja kwa mwengine. Kama vile Kristo aliwasamehe, musameheane pia. Lakini zaidi ya mambo hayo yote muvae upendo, ambayo ni kifungo cha ukamilifu” (Wakolosayi 3:12-14).
Kitendo cha mwisho cha Mungu kitafungwa kwa mvua ya kwanza na ya nyuma ambayo imehaidiwa mbele ya kurudi kwa Kristo na waamini wa kweli watakuwa wenye roho moja na nafsi moja: “Muwe sasa wavumilivu, wandugu mpaka kuja kwa Bwana. tazama, mukulima anangoja tunda la kweli la udongo, akiwa muvumilivu kwa hiyo, mpaka aweze kupokea mvua ya kwanza na ya mwisho.” (Yakobo 5:7).
“Mulisikia ikisemeka kuhusu uvumilivu ya Yobu, namuliona mwisho ambayo Bwana Aliyo mupa, kwa maana Bwana Anajaa rehema na upendo” (Yakobo 5:10-11)
Tuwe sasa wavumilivu, kama vile Yobu, ambae maana yake katika kiebrania mwenye kuteswa, yeye ambae nyuma ya majaribu kali ikamuonyesha Mungu zaidi kwa nguvu kuliko mbele. Tusinungunikiane tena wamoja kwa wengine, lakini tuishi na kudumu mpaka kuja kwa Bwana. Mungu Ambae ni mwaminifu Atatubariki kama vile Aliyafanya kwa Yobu ikiwa mfano. Wote ambawo walimuelewa vibaya na kumushitaki waliikala sasa pamoja nae kwa meza moja. Tunajuwa kwa uhakika ya kwamba Mukombozi wetu Anaishi na Atafikisha kwa uzuri mambo yote kwa ukamlifu. Wote ambawo wamebaki waaminifu na hawakujiachilia kudanganywa watayaishi.
“Bwana Akamurudisha Yobu katika hali yake ya kwanza, wakati Yobu alipo waombea marafiki zake; na Bwana Akamupatia mara mbili ya yote ambayo aliyo kuwa nayo. Wandugu, wadada, na marafiki wa zamani wa Yobu akawaona wote wakimutembeleya, na wakakula pamoja naye katika nyumba yake. Wakamupa pole na kumufariji kwa ajili ya shida zote ambazo Bwana Alikuwa Ameleta juu yake, na kila moja akamupa kesita moja na pete ya zahabu” (Yobu 42:10-11).